Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

OFISI YA MWANDISHI MKUU WA SHERIA

Majukumu ya Divisheni ya Ufasiri wa Kisheria

.

Divisheni inaongozwa na Mkurugenzi na ina Sehemu mbili (2) zifuatazo:

  1. Sehemu ya Ufasiri wa Sheria Kuu; na
  2. Sehemu ya Ufasiri wa Sheria Ndogo.

Lengo

Kutoa huduma zinazohusiana na tafsiri ya sheria na tafsiri ya hati nyingine za kisheria.

Majukumu

Divisheni hii inatekeleza majukumu yafuatayo:

  1. Kushauri wizara, idara zinazojitegemea, wakala za serikali, mamlaka za serikali za mitaa na taasisi nyingine za serikali kuhusiana na masuala ya tafsiri za kisheria.
  2. Kutafsiri sheria na hati za kisheria kutoka lugha ya Kiswahili kwenda lugha ya Kiingereza na kinyume chake.
  3. Kutafsiri hati nyingine za kisheria katika lugha nyingine yoyote inayohitajika.
  4. Kuhakiki sheria zilizotafsiriwa.
  5. Kuandaa na kupitia nyenzo na zana za tafsiri ya sheria.
  6. Kutoa ushauri na mwongozo kuhusu tafsiri ya sheria kwa wizara, idara zinazojitegemea, wakala za serikali, mamlaka za serikali za mitaa na taasisi nyingine za serikali.
  7.  Kuandaa na kutekeleza mpango wa tafsiri ya sheria kwa mwaka wa fedha na kumshauri ipasavyo Mwandishi Mkuu wa Sheria.
  8.  Kuratibu mikutano ya ushirikishwaji wa wadau wakati wa mchakato wa tafsiri ya sheria.
  9. Kushauri na kusimamia uchapishaji wa sheria zilizotafsiriwa katika Gazeti la Serikali.
  10.  Kuhakikisha usahihi na mfanano wa sheria zilizotafsiriwa kwa kuzingatia kanuni za uandishi wa sheria.
  11.  Kuandaa, kutunza na kuendeleza rejesta ya sheria zilizotafsiriwa.