Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

OFISI YA MWANDISHI MKUU WA SHERIA

Mwandishi Mkuu wa Sheria
Bw. Onorius John Njole
Mwandishi Mkuu wa Sheria

Sisi ni Nani

Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria (OCPD) ina jukumu la msingi la kubadili sera kuwa sheria ambazo zinasaidia upatikanaji wa haki, usawa na maendeleo. Watumishi wetu ambao ni waandishi wa sheria, mawakili wa serikali, warekebu wa sheria, makatibu sheria na watumishi wengine ni msingi wa kazi zetu, wakileta utaalamu, uadilifu na kujitolea katika kila jukumu la kutunga sheria. Tangu ilipoanzishwa kama sehemu ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, OCPD imeendelea kutekeleza maono ya dira yake kuwa kitovu cha ubora katika uandishi wa sheria. Jukumu letu huanza pale ambapo hitaji la sheria linapotambuliwa na tunaendelea kushiriki kikamilifu katika mchakato mzima wa uandishi wa sheria, vikao vya Bunge na hata baada ya sheria kupitishwa, tunahakikisha kwamba sheria zilizotungwa zinakidhi kwa ufanisi. Huduma zetu zinalenga kutoa sheria bora, zinazopatikana kwa urahisi na kwa usahihi kwa ajili ya kujenga msingi imara kwa maendeleo endelevu. Zaidi ya uandishi wa sheria, tunashirikiana kwa karibu na Bunge, Mahakama, taasisi za serikali na wadau wengine kuhakikisha kuwa sheria zinapatikana kwa lugha rahisi ili kukidhi dhamira yetu ya upatikanaji wa sheria bora kwa kila mtu. OCPD pia imedhamiria kukuza ushirikiano utakaochangia uthabiti wa kiuchumi, ukuaji wa maendeleo na haki za binadamu na kujenga msingi endelevu.  

Kutoka kwa Dawati la CPD

MaadiliMsingi

First slide
Tunahimiza uwazi, uaminifu na uwajibikaji kwa kila mtumishi katika kutekeleza majukumu ya Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria. Kila mtumishi anatak...
Uwazi na Uwajibikaji
First slide
Tunahakikisha kuwa tunashirikisha na kufanya kazi pamoja na wadau mbalimbali katika kutimiza majukumu yetu.
Ushirikiano
First slide
Tumejitoa katika kutumia viwango vya juu vya ujuzi, maarifa na umahiri kwa watumishi wote katika utekelezaji wa majukumu yao.
Utaalamu
First slide
Tunahakikisha kuwa sheria zote zilizoandikwa, zilizotafsiriwa, zilizorekebiwa na nyaraka nyingine za kisheria zilizoandaliwa kwa ajili ya kuridhiwa zi...
Upatikanaji
First slide
Tunazingatia uaminifu, kanuni thabiti za maadili na bidii katika kuhudumia taifa. Daima tunajitahidi kuzingatia kanuni za utawala bora.
Uadilifu