Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

OFISI YA MWANDISHI MKUU WA SHERIA

Kitengo cha Ununuzi na Ugavi

.

Kitengo kinaongozwa na Mkuu wa Kitengo cha Ununuzi na Ugavi.

Lengo

Kutoa utaalamu katika huduma za ununuzi na ugavi.

Majukumu

Kitengo kinatekeleza majukumu yafuatayo: 

  1. Kumshauri Afisa Masuuli kuhusu masuala yote yanayohusiana na ununuzi.
  2. Kusimamia shughuli zote za ununuzi na uondoshaji kwa njia ya zabuni isipokuwa uamuzi wa zabuni na utoaji wa mkataba.
  3. Kutekeleza maamuzi ya bodi ya zabuni.
  4. Kupendekeza manunuzi na uondoshaji kwa taratibu za zabuni.
  5. Kuratibu utayarishaji wa taarifa za mahitaji.
  6. Kuandaa nyaraka za zabuni.
  7. Kuandaa matangazo ya fursa za zabuni.
  8. Kuandaa na kutoa nyaraka za mikataba zilizosainiwa.
  9. Kutunza taarifa za ununuzi kwa ajili ya kumbukumbu na taratibu za uondoshaji.
  10. Kutunza orodha au rejesta ya mikataba yote iliyotolewa.
  11. Kuandaa na kuwasilisha kwa menejimenti taarifa za robo mwaka za utekelezaji wa mpango wa ununuzi wa mwaka.
  12. Kuandaa na kutekeleza mpango wa ununuzi wa mwaka.
  13. Kufuatilia uzingatiaji wa mchakato na taratibu za ununuzi kwa mujibu wa Sheria ya Ununuzi wa Umma.
  14. Kusimamia na kufuatilia ununuzi wa vifaa vya ofisi.
  15. Kuendeleza na kusasisha orodha ya bidhaa na vifaa.
  16. Kufanya kazi kama sekretarieti ya bodi ya zabuni.
  17. Kuandaa vigezo msawazo au viwango vya huduma na bidhaa zinazonunuliwa na kuzingatia thamani ya fedha.
  18. Kuandaa na kuwasilisha taarifa za utendaji kwa Mwandishi Mkuu wa Sheria.