Majukumu ya Kitengo cha Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
Majukumu ya Kitengo cha Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
.
Kitengo kinaongozwa na Mkurugenzi.
Lengo
Kutoa utaalam juu ya usimamizi wa rasilimaliwatu na masuala ya utawala.
Majukumu
Kitengo kinatekeleza majukumu yafuatayo:
- Kutafsiri Kanuni za Utumishi wa Umma, Kanuni za Kudumu, na Sheria nyingine za Kazi.
- Kusimamia maadili na kuhamasisha shughuli zinazoongeza thamani kwa watumishi.
- Kumshauri Afisa Masuuli kuhusu masuala yanayohusiana na rasilimali watu na utawala.
- Kuhakikisha usimamizi na matumizi bora, yenye ufanisi na tija wa rasilimali watu.
- Kuratibu utekelezaji wa malengo ya taasisi kwa ngazi ya mtu mmoja mmoja na timu.
- Kuwezesha mafunzo ya watumishi na maendeleo ya taaluma.
- Kukusanya, kuchambua, kuhifadhi, na kusambaza takwimu na taarifa zinazohusiana na mipango ya maendeleo ya rasilimali watu.
- Kutoa takwimu na kusasisha kumbukumbu za taarifa mbalimbali za rasilimali watu.
- Kuratibu Baraza la Wafanyakazi.
- Kuratibu utatuzi wa malalamiko.
- Kuwezesha mahusiano ya wafanyakazi na ustawi wao, ikiwemo afya na usalama kazini, michezo na utamaduni.
- Kutoa huduma za kumbukumbu, usafirishaji wa nyaraka na mizigo.
- Kushughulikia masuala ya itifaki.
- Kuwezesha upatikanaji wa huduma za ulinzi, usafiri, na mahitaji ya jumla.
- kuwezesha matengenezo ya vifaa vya ofisi, majengo na maeneo ya ofisi.
- Kuratibu utekelezaji wa masuala anuwai.
- Kuratibu utekelezaji wa ushiriki wa sekta binafsi, maboresho ya mchakato wa kazi, na Mkataba wa Huduma kwa Wateja.
- Kuandaa taarifa za utendaji.