Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

OFISI YA MWANDISHI MKUU WA SHERIA

Majukumu ya Kitengo cha Mipango na Bajeti

.

Kitengo kinaongozwa na Mkuu wa Kitengo.

Lengo

Kutoa utaalamu katika mipango, bajeti na utafiti. 

Majukumu

Kitengo kinatekeleza majukumu yafuatayo:

  1. Kumshauri Afisa Masuuli kuhusu masuala yote yanayohusiana na mipango na bajeti.
  2. Kuratibu maandalizi, kupitia na kutekeleza mpango mkakati, mipango ya kila mwaka na bajeti.
  3. Kutoa maoni kwenye hotuba ya bajeti ya wizara na ripoti ya uchumi ya kila mwaka.
  4. Kujumuisha ujuzi wa masuala ya mpango mkakati na bajeti kuwa sehemu ya mfumo wa taasisi.
  5. Kuchambua miongozo ya bajeti na kuandaa bajeti ya taasisi inayoakisi mpango na bajeti ya Serikali.
  6. Kuratibu maandalizi, ukusanyaji wa rasilimali na utekelezaji wa miradi au programu za maendeleo.
  7. Kuratibu utengenezaji na uandaaji wa mpango wa mwaka na mpango mkakati wa kati.
  8. Kuunganisha miradi, programu, mipango ya utekelezaji na kuandaa mikakati ya ukusanyaji na ugawaji wa rasilimali.
  9. Kutoa mchango katika uanzishaji wa utekelezaji wa malengo na viashiria.
  10. Kutoa mwongozo wa kitaalamu na kuwezesha mchakato wa upangaji mkakati na uandaaji wa bajeti katika mifumo rasmi ya taasisi.
  11. Kukusanya, kujifunza na kuchambua takwimu kwa ajili ya kuandaa na kutekeleza sera, mipango na mapendekezo ya bajeti.
  12. Kuandaa na kuwasilisha taarifa za utendaji kwa Mwandishi Mkuu wa Sheria.