Majukumu ya Kitengo cha Udhibiti Ubora
Majukumu ya Kitengo cha Udhibiti Ubora
.
Kitengo kinaongozwa na Mkuu wa Kitengo.
Lengo
Kuhakikisha kwamba sheria na nyaraka zinazohusiana zinazoandaliwa na Ofisi zinakidhi malengo na viwango vya usahihi,mfanano na uhalali.
Majukumu
Kitengo kinatekeleza majukumu yafuatayo:
- Kumshauri Mwandishi Mkuu wa Sheria (CPD) kuhusu viwango na ubora wa nyaraka na huduma za uandishi wa sheria.
- Kupitia sheria zilizohakikiwa ili kuhakikisha zinaendana na viwango na kanuni zilizowekwa za uandishi wa sheria.
- Kuratibu uanzishwaji na uendelezaji wa viwango na kanuni za uandishi wa sheria.
- Kufanya tathmini ya athari za sheria baada ya kutungwa na athari za udhibiti na usimamizi.
- Kuanzisha mfumo wa uhakiki ubora.
- Kupitia miongozo ya uandishi wa sheria na kutoa mapendekezo kwa Divisheni husika kuhusu kanuni za uandishi na maendeleo yake.
- Kushauri juu ya maboresho ya nyenzo na zana za uandishi wa sheria.
- Kufanya uhakiki wa mwisho wa nyaraka za kisheria kabla ya kuchapishwa.
- Kutambua na kushauri kuhusu maeneo yanayopaswa kuzingatiwa wakati wa kuandaa, kupitia, na kuhakiki nyaraka za sheria.
- Kupendekeza maeneo ya maboresho na kujenga uwezo na kushauri ipasavyo kwa lengo la kuboresha ubora wa nyaraka za sheria.
- Kuandaa taarifa za utendaji kazi.